April 11, 2015

MSOLLA (KUSHOTO) AKIWA NA RAIS JAKAYA KIKWETE.


Siku kadhaa baada ya Taifa Stars kupangwa Kundi G na Nigeria, Misri na Chad katika kuwania kufuzu Kombe la Afrika 2017, kocha wa zamani wa timu hiyo, Mshindo Msolla amesema kikosi hicho hakitafuzu kwani mwalimu wake anapoteza muda tu nchini.

Msolla ambaye ndiye kocha wa mwisho kuifundisha Taifa Stars kabla ya ujio wa Marcio Maximo mwaka 2006, aliliambia Championi Jumamosi kuwa, Tanzania haitafanya vizuri kwani kocha wake Mart Nooij hana mtazamo wa kimaendeleo na soka la nchi hii.

Alisema Nooij hajafanya jambo lolote la msingi kuhakikisha Taifa Stars inapiga hatua, badala yake anasubiri mkataba wake uishe aondoke.

 “Hatutafanya lolote mbele ya mataifa kwa sababu ya kocha wetu wa sasa wa Taifa Stars, hana mtazamo wa kimaendeleo wa soka la nchi hii,” alisema Msolla.

“Tangu amefika hakuna alichokifanya cha maana kwa ajili ya timu na soka la Tanzania, badala yake anaangalia mshahara wake mzuri na kulinda CV yake isichafuke tu.”

Taifa Stars itaanza na Misri kati ya Juni 12 na 14, mwaka huu kufuzu Kombe la Afrika 2017.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic