April 17, 2015

NGASSA&MSUVA...
Kiungo wa zamani wa Yanga, Edibily Jonas Lunyamila ameibuka na kuwapa mbinu za kuwaondoa Etoile du Sahel ya Tunisia kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kuwa ni kuhakikisha kesho wanashinda kuanzia mabao matatu.


Lunyamila amefunguka kuwa siku zote asili ya soka la Waarabu ni kucheza kwa tahadhari kubwa na kujilinda ili wakusubirie kwao, hivyo kuwataka Mrisho Ngassa, Simon Msuva wa Yanga na wenzao kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa nyumbani.
 
LUNYAMILA...
Lunyamila amesema Yanga wanatakiwa kutumia mwanya huo kujihakikishia wingi wa mabao kwa kile anachoamini ugenini ni pagumu kutoka.


“Waarabu wanajulikana. Wanapokuwa ugenini wanataka kupunguza idadi ya mabao, hivyo hucheza soka la kujilinda zaidi- wanasaka sare tu ili wakusubirie kwao,” alisema winga huyo aliyetikisa miaka ya 1990.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic