April 17, 2015


Siku chache tangu aliyekuwa kocha wa muda wa Polisi Morogoro, Amri Said atangaze kubwaga manyanga kuifundisha timu hiyo, imebainika kuwa Yanga ndiyo chanzo.


Amri anadaiwa kufanya hivyo kutokana na kuhofia kipigo kutoka kwa Yanga kama ilichokumbana nacho Coastal Union ya Tanga cha mabao 8-0, kwa kuwa Yanga inatarajiwa kucheza na Polisi Moro hivi karibuni.

Amri alisema kukosa ushirikiano klabuni hapo ni sababu kubwa ya kujiondoa huku ikizingatiwa kuwa timu hiyo ipo katika nafasi mbaya kwenye Ligi Kuu Bara.

“Kila nililokuwa nikiwaambia waliona ni jambo la kawaida wakati timu ipo kwenye nafasi mbaya, nikaona ni bora nijiondoe kuliko kuja kuharibu CV yangu na ukizingatia timu hiyo bado hajacheza na Yanga, yasije kunikuta kama yaliyomkuta ndugu yangu Julio (Jamhuri Kihwelo, kocha wa Coastal),” alisema Amri.




1 COMMENTS:

  1. Hahahahahahahahaha,jamani Yanga mnatisha!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic