April 7, 2015


Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime amesema ana imani kikosi chake kitainuka.


Maxime amesema wamekuwa wakipoteza mechi mfululizo, hali inayowashangaza lakini wanaamini ndiyo matokeo ya mpira.

“Kila kitu chetu kipo vizuri, tunafanya mazoezi vizuri na mambo yote yako vizuri. Lakini kinachotokea mbele yetu, kila mmoja kinamshangaza.

“Ambacho tunaangalia mbele ni kuhakikisha tunashinda na kupata pointi tatu muhimu,” alisema Maxime.
Mtibwa Sugar imebakiza mechi sita huku ikiwa katika nafasi ya 14 katika msimamo wa Ligi Kuu Bara.


Mtibwa ilimaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ikiwa kileleni huku ikiwa imecheza mechi nane bila ya kupoteza moja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic