April 11, 2015


Uongozi wa Simba umefikia kwenye makubaliano na beki wake Hassan Kessy kupitia kwa meneja wake.


Kessy alijiondoa katika kikosi cha Simba akishinikiza kulipwa haki zake kwa mujibu wa mkataba ikiwemo shilingi milioni 5 za sehemu ya dau la usajili na nyumba ya kuishi kama walivyokubaliana na uongozi alipojiunga nao Desemba, mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar.

Meneja wa Kessy, Athuman Tippo ‘Zizzou’ amesema; “Jana (juzi Alhamisi) mchana viongozi wa Simba walinipa fedha za kodi ya nyumba ya Kessy.

“Sasa tupo katika mchakato wa kutafuta nyumba nzuri ya kuishi mchezaji wangu, ila kuhusu zile fedha nyingine (milioni 5) wametuomba muda wa kumalizia na tumewakubalia.”

Tippo ambaye amewahi kuichezea Coastal Union ya Tanga, alisema uamuzi wa Kessy kujiondoa katika kikosi cha Simba ulikuwa sahihi kwani alikuwa anadai haki yake ya msingi.


Kessy alithibitisha kupokea kiasi hicho cha fedha kutoka Simba kwa kusema; “Nilikuwa Morogoro lakini sasa nipo Dar na fedha tumelipwa, hivyo natarajia kujiunga na Simba mapema wiki ijayo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic