April 27, 2015


Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe, ameitupia dongo kiaina timu yake ya zamani ya Simba akisema anashukuru kwa kuwa yupo Yanga ambako ana nafasi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara lakini kama angeendelea kukaa Msimbazi, asingepata nafasi hiyo.


Msimu uliopita, Tambwe alikuwa Simba na kuibuka mfungaji bora kwa kufunga mabao 19 lakini alishindwa kupata ubingwa huo, baada ya timu yake kushika nafasi ya nne.

Yanga sasa inaongoza ligi ikiwa na pointi 52 na kama leo itafanikiwa kuibuka na ushindi katika mchezo dhidi ya Polisi Moro kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, itakuwa tayari imeubeba ubingwa huo unaoshikiliwa na Azam FC.
Akizungumzia kuchukua ubingwa wa kwanza wa ligi kuu, Tambwe amesema atafurahia kuchukua ubingwa huo kwa mara ya kwanza akiwa na Yanga baada ya kushindwa kufanya hivyo akiwa Simba, ingawa alidumu klabuni hapo kwa muda mrefu.

“Ninamshukuru Mungu msimu huu kwa kuwa nitafanikiwa kuchukua ubingwa nikiwa na Yanga, ni jambo la faraja sana kwangu kwa sababu nilifeli nikiwa Simba, ingawa nilikaa kwa msimu mzima, lakini hapa Yanga nina muda mchache tu tangu nijiunge nao.


“Hii ni historia nzuri kwangu na inanifanya niwe na faraja kwa sababu kila mchezaji anapambana ili kupata mafanikio, ikiwemo mataji, ndiyo maana ninajituma sana uwanjani, kama nisipofunga basi nitoe pasi ya bao,” alisema Tambwe ambaye mpaka sasa ameifungia Yanga mabao 11 katika Ligi Kuu Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic