April 29, 2015


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda leo amekabidhiwa vifaa vya michezo kutoka kwa kampuni ya Tanzania Kwetu Nyumbani (TSN).


Kampuni hiyo maarufu kwa uuzaji bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta ta petroli na dizeli, imetoa vifaa kupitia vinywaji vya Chilly Willy na Smart Sports, vitakavyotumika kwenye mashindano yaliyoandaliwa na Manispaa ya Wilaya ya Kinondoni, yatakayojulikana kama Kinondoni Cup.

Vifaa alivyokabidhiwa ni jezi za mpira wa miguu seti 60, jezi za netiboli 40, pamoja na mipira 100, vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Milioni 50.

 Akizungumza na waandishi wa habari, Makonda alisema kuwa anazishukuru kampuni hiyo kwa kutoa vifaa hivyo ambavyo vitatumika kwenye mashindano hayo yatakayoshirikisha timu kutoka kata zote 34 za wilaya hiyo.

“Hii ni dalili ya kuonyesha kuwa wemeniunga mkono, hivyo ni lazima niwashukuru katika hili, kazi imebaki kwa timu kujitokeza kushiriki.

“Katika mpira wa miguu wanaume tutachukua timu mbili kutoka kila kata, netiboli timu moja katika soka la wanawake tunatarajia kupata timu 18, na timu zote hizo zitapewa vifaa,” alisema Makonda.

Kwa upande wake mwakilishi wa TSN, Hamisi Tembo alisema, “Tumeamua kumuunga mkono katika hili baada ya kuona jambo alilolianzisha lina faida kwa vijana pamoja na taifa, tunaamini vifaa hivyo vitasaidia kuyafanikisha mashindano haya.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic