April 29, 2015


Mwanachama wa Yanga ambaye ni mlezi wa  Kundi la Yanga International Supporter (YIS), Madaraka  Marumbo, juzi alimkabidhi viatu maalum nahodha wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambavyo atavitumia kwenye mchezo wa kimataifa dhidi ya Etoile du Sahel.


Cannavaro alikabidhiwa viatu hivyo mara baada ya mchezo dhidi ya Polisi Moro juzi ingawa hakuweza kucheza kwenye mchezo huo kutokana na kuandamwa na majeraha.

 Kiongozi huyo alifunguka na kusema kuwa aliamua kutoa zawadi hiyo kutokana na kuthamini mchango wa nahodha huyo kwenye timu hiyo.

“Niliamua kumpa zawadi hiyo kwa kutambua mchango wake na nikiwa kama shabiki wake pamoja na timu kwa ujumla. Nafahamu wana mchezo mkubwa mbele yao, hivyo wanatakiwa kujituma kwa bidii na kuweza kuwashangaza Waarabu hata kama watakuwa ugenini,” alisema Marumbo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic