April 26, 2015

Unaweza kusema bora hata wale wanaofanya vurugu Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam zinapokutana Simba na Yanga.


Mechi za watani zina mambo, si kwamba tunawasapoti waendelee na vurugu lakini hizi zilizotokea jana kule Belgrade mji mkuu wa Serbia zilikuwa hatari.
Watani Red Star Belgrade na Partizan Belgrade walikuwa wanakutana, aisee ilikuwa ni hatari ile mbaya.
Pamoja na mechi kwisha kwa sare ya 0-0 lakini Polisi walichapana na mashabiki ile mbaya.

Kwanza walianza mashabiki wa timu hizo, Polisi walipoingilia, wao wakawavamia na kuanza kuwatandika ilivyo.

Polisi waliokuwa kwenye Uwanja wa Red Star waliopoona wanazidiwa wakaanza kurusha mabomu ya machozi.

Mwisho mashabiki zaidi ya 50 waliumia, 41 wakakamatwa na kutiwa nguvuni na askari 35 wakajeruhiwa.
PICHA ZINASIKITISHA, TUNAWAOMBA RADHI LAKINI LENGO UONE ILIVYOKUWA.












0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic