May 12, 2015

ADEBAYOR AKIWA NA ROTIMI...
Emmanuel Adebayor ameendelea kuibua madudu ya ndugu zake baada ya kusema mdogo wake aliiba jezi zake mbili alizokuwa amepewa na nyota wakubwa duniani.

Adrbayor amesema mdogo wake wa mwisho aitwaye Rotimi aliiba jezi mbili alizopewa na Marc-Vivien Foe na gwiji wa Real Madrid, Zinedine Zidane.

Pia Rotimi alishirikiana na rafiki zake kuiba mkufu wenye thamani ya pauni 25,000 aliomnunulia mama yake.
Kijana huyo, ndiyo yule aliyemuelezea mwanzo kwamba aliiba simu za wachezaji 21 alipomlipia kwenye akademi apate mafunzo nchini Ufaransa.

Adebayor amekuwa akitema ‘nyongo’ kuhusiana na ndugu zake ambao awali walianzisha kumlaumu.


Aidha, alisimulia kuwa mdogo wake huyo pia aliiba vifaa mbalimbali kwa wenzake ikiwamo kutoka kwa mtoto wa nyota wa zamani wa Cameroon, Jack Song’oo na kusababisha uhusiano wake na familia ya mchezaji huyo kuzorota.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic