May 9, 2015

TELELA
Kiungo wa Azam, Frank Domayo  ameshindwa kujizuia na kujikuta akimpongeza Salum Telela wa Yanga kwa kusema jamaa anajua na ametoa mchango mkubwa katika ubingwa wa Ligi Kuu Bara wa Wanajangwani msimu huu.


Domayo amesema: “Telela anajua sana, kwa siku za hivi karibuni nimeona anacheza vizuri pale katikati na kama hatosumbuliwa basi atafika mbali katika maisha yake ya soka.”
DOMAYO WAKATI AKIICHEZEA YANGA
Jumatano iliyopita wawili hao walionyesha ufundi wa hali ya juu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati timu zao zilipopambna ambapo Azam ilishinda mabao 2-1.


Telela alionekana kumzidi maarifa Domayo kila mara katika mchezo huo uliochezwa dakika zote kwenye mvua na uwanja kuharibika sehemu ya kuchezea ‘pichi’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic