May 9, 2015


Mkongwe Ivo Mapunda wala hana papara ya usajili katika klabu yake ya Simba kwani mabosi wake wamemuahidi kumuongezea mkataba ambao mwenyewe anataka uwe wa miezi 18 tu.


Ivo, kipa mzoefu katika Ligi Kuu Bara, alitua Simba msimu wa 2013/14 akiwa chaguo la kwanza kwa Kocha Zdravko Logarusic na wa sasa Goran Kopunovic, mkataba wake unaisha Mei 20, mwaka huu.

Ivo, alisema bado hajasaini mkataba wowote na timu hiyo kwani anawasubiri viongozi wake waliomhakikishia kumsainisha siku yoyote kuanzia sasa.

“Kwa sasa nawasubiri viongozi wa Simba ambao waliniahidi kuniongezea mkataba, nitasaini mkataba wa mwaka mmoja na miezi sita tu. Unajua mimi ni mchezaji ninayejali maslahi sana, nadhani mkataba mfupi ni mzuri katika kuongeza thamani yako kama mchezaji,” alisema Ivo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic