May 9, 2015

Kiungo nyota wa Manchester United, Marouane Fellaini hatimaye ameamua kufunguka na kuelezea alivyomwaga chozi baada ya kupata uhakika kocha David Moyes alikuwa ametimuliwa kazi.


Fellaini raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Uarabuni, amesema alishindwa kujizua na kumwaga chozi baada ya kugundua kocha huyo kweli alikuwa amefukuzwa kazi Aprili, mwaka jana.
“Nimefanya kazi miaka sita na Moyes, kwangu alikuwa kama mzazi na alinisaidia sana. Mimi ni binadamu, sikuwa na ujanja namachozi yalimwagika.

“Unajua nilisikia kwenye vyombo vya habari siku moja kabla lakini sikuwa na uhakika kama ni kweli au la.

“Siku iliyofuata nilipofika mazoezini nilikwenda kwenye mgahawa, baadaye nikamuona Moyes akiwa amevaa suti na si suti (trak suti), nikajua ni kweli.

“Baadaye alinifuata na kunichukua hadi ofisini kwake ambako kule alinieleza ukweli kuhusiana na kuondoka kwake huku akinisisitiza huo ndiyo mpira ulivyo, nililia,” anaeleza Fellaini.

Moyes ndiye alimsajili Fellaini kutoka Everton ambayo aliifundisha kwa muda mrefu zaidi na kumfanya kuwa kocha wa tatu kwa kudumu katika klabu moja kwa muda mwingi nchini England baada ya Alex Ferguson na Manchester United na Arsene Wenger na Arsenal.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic