May 11, 2015


Kocha machachari, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, amefunguka kuwa yupo tayari kufundisha timu yoyote kati ya Coastal Union na Mwadui FC kwa kuangalia dau atakalopatiwa na timu hizo mbili msimu ujao.


Julio alifanikiwa kuipandisha Mwadui ligi kuu lakini baada ya hapo akaombwa kuiongezea nguvu Coastal Union kwa muda lakini Wagosi hao wa Kaya wamenogewa naye na wanataka aendelee kuwa nao.

Julio amesema kwa upande wake yupo tayari kufundisha timu yoyote kati ya Mwadui na Coastal kwa kuwa anaangalia maslahi zaidi na si vinginevyo.

“Kwa sasa bado sijaamua nitakuwa wapi msimu ujao kati ya timu yangu ya Mwadui na Coastal Union, lakini nitaangalia timu ambayo itanipa maslahi mazuri, kwani kufundisha ndiyo kazi yangu,” alisema Mwadui.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Mwadui, Omary Khatibu, alisema kuwa kwa upande wao wanamsubiri kocha huyo atoe maamuzi iwapo ataendelea na timu hiyo au la kwa kuwa hadi sasa hawana kocha.


“Sisi tunamsubiri Julio ambaye tumekubaliana aje huku baada ya wiki mbili kuanzia sasa, hivyo yeye ndiye atakayetoa mapendekezo juu ya wachezaji atakaotaka kuwasjili msimu ujao.

“Lakini kwa ujumla wachezaji tutakaoendelea nao ni wale walioipandisha timu na baadhi kutoka ligi kuu ambapo tumeshafanya nao mazungumzo na mambo yakikamilika tutaweka wazi kila kitu.

“Kuhusu Julio, tunasubiri jibu lake kama atataka kuendelea tutaendelea naye na kama akikataa, basi tutamuacha na kutafuta kocha mwingine,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic