May 11, 2015

HIKI NDICHO KIKOSI CHA ETOILE WANACHOTAKIWA NGASSA NA TWITE
Wachezaji wa Yanga sasa wameonekana kuwa lulu kufuatia viwango walivyovionyesha katika michuano ya kimataifa ambapo timu za Etoile du Sahel ya Tunisia, Platinum ya Zimbabwe na BDF ya Boswana zimevutiwa na wachezaji watano wa timu hiyo.


Mrisho Ngassa na Mbuyu Twite ndiyo wanaonekana kuwa chaguo la kwanza kwa timu ya Etoile du Sahel.
NGASSA.
Yanga iliondolewa katika michuano ya kimataifa hivi karibuni dhidi ya Etoile du Sahel kwa jumla ya mabao 2-1 huku ikiwa imeacha gumzo kwa wapinzani wao hao kutokana na kuonyesha ushindani wa hali ya juu licha ya kutolewa mashindanoni.

Wachezaji ambao wamezitoa udenda timu hizo ni Amissi Tambwe, Mbuyu Twite, Mrisho Ngassa, Haruna Niyonzima na Kpah Sherman.

Chanzo kutoka ndani ya Yanga kimeeleza kuwa, viongozi wa timu hizo waliwataarifu juu ya kuwahitaji wachezaji hao kwa ajili ya kufanya biashara.

“Timu za Etoile, Platinum na BDF tulizokutana nazo zimetoa ofa ya kuwahitaji wachezaji wetu kwa lengo la kuwanunua kutokana na kuvikubali viwango vyao ambapo kila timu imetaja wachezaji wake inaowaona wanafaa.
      
“Wachezaji waliotajwa na timu hizo ni Tambwe ambaye timu mbili za Platinum na Etoile zimevutiwa naye, Mbuyu Twite, Niyonzima na Ngassa ambao wote wanatakiwa na Etoile huku Sherman akitakiwa na BDF.


“Kwa upande wa uongozi wenyewe hawajakataa wala kukubali ofa hizo ambapo waliwataka wasubiri hadi wamalize mechi zao za kimataifa mbapo tayari wameshatolewa ikiwa ni pamoja na ligi kumalizika, hivyo wakati wowote kuanzia sasa timu hizo zitaleta maombi rasmi ya kuwahitaji wachezaji hao,” kilisema chanzo hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic