May 9, 2015


Azam FC imefikiria kuhusu straika wake, Didier Kavumbagu kutingisha kiberiti na kutaka kurudi Yanga, kisha ikasema wala hakuna shida aende tu.


Siku kadhaa nyuma mabosi wa Yanga waliokuwa katika harakati za kumshawishi Kavumbagu arejee kwenye kikosi chao ili kuimarisha safu ya ushambuliaji na Azam ilikuwa kimya tu.

Kaimu Kocha wa Azam, George ‘Best’ Nsimbe ametoa mkono wa baraka kwa mchezaji huyo kuangalia mbele zaidi kwa manufaa yake endapo anadhani Yanga ni mahali sahihi kwake.

Nsimbe alisema: “Siwezi kumkataza mchezaji kuondoka kama ameamua, lakini huyu ni mchezaji muhimu kwetu na ningependa abaki.

“Nitajitahidi kumshauri abaki lakini kama ataamua mwenyewe kuondoka, basi aende tu maana moyo wake utakuwa umependa kufanya hivyo. Naamini wapo wanaoweza kucheza nafasi yake,” alisema kocha huyo wa zamani wa KCCA ya Uganda.

Habari kutoka ndani ya Yanga zinasema uongozi unafanya jitihada zote kuhakikisha Kavumbagu anasajiliwa kwani ni chaguo la Kocha Hans van der Pluijm ambaye hana mshambuliaji wa uhakika katika kikosi chake.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic