May 12, 2015

Kocha Jose Mourinho wa Chelsea anajulikana kwa utukutu. Lakini bado unaweza kumsifia kutokana na ubora wa mambo mengine kwa kuwa mwelewa.


Wakati kiungo mkongwe na gwiji wa Liverpool, Steven Gerrard alipotolewa katika mechi dhidi ya Chelsea, Mourinho na mashabiki wa Chelsea walisimama na kumpigia makofi.

Mashabiki hao walimpigia makofi Gerrard ikiwa ni kama kumuaga kwa kuwa ndiyo mechi yake ya mwisho akiwa na Liverpool dhidi ya Chelsea kwenye Uwanja wa Stamford Brigdge.

Kumbuka, Gerrard wakati anatoka, alikuwa ndiye aliyefunga bao la kusawazisha dhidi ya Chelsea na matokeo yalikuwa 1-1 wakati huo, hadi mwisho wa mchezo.


Kuna kila sababu ya kuona Mourinho ni muelewa kwa kuwa aliwaongoza mashabiki hao wa Chelsea kupiga makofi hao ya pongezi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic