May 13, 2015

TAMBWE AKIWA NA MWANAYE
Straika nyota wa Yanga, Amissi Tambwe, ameondoka nchini jana kwenda kwao, Burundi kwa ajili ya kuonana na familia yake ambayo hivi sasa ipo katika wasiwasi mkubwa kutokana na vurugu za kisiasa zinazoendelea nchini humo.


Tambwe amesema kuwa imembidi aende nchini humo ili aweze kuona ni jinsi gani ataisaidia familia yake hiyo ambayo haina tena amani kama ilivyokuwa hapo zamani.

“Sina jinsi, imenibidi niende ila ni matumaini yangu nitafika salama na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu nitajipatia ujasili wa kuweza kuisaidia familia yangu.

“Nimekuwa nikiwasiliana nayo kila wakati lakini hofu ndiyo jambo kubwa lililotawala nafsi zao, jambo ambalo pia hata mimi linaniumiza na zaidi kila ninapowaona Warundi wanzangu wakikimbia kuja Tanzania kuomba msaada wa hifadhi.

“Ikiwezekana naweza kuja nao ili niishi nao hapa (Tanzania) kwa amani, nawaomba ndugu zangu wa Yanga na Watanzania wote waniombee nifike salama na niweze kuisaidia familia yangu,” alisema Tambwe.

Machafuko ya kisiasa nchini Burundi yanatokana na uamuzi wa rais wa nchi hiyo, Pierre Nkurunzinza kutangaza kuwania nafasi ya kugombea urais ili aingie madarakani kwa awamu ya tatu, jambo ambalo linapingwa vikali na wapinzani wake.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic