May 13, 2015


Baada ya kufanikiwa kusalia katika Ligi Kuu Bara ukiwa ni msimu wake wa kwanza kushiriki ligi hiyo, uongozi wa Stand United umejipanga kuhakikisha unatenga shilingi milioni 350 ili kusajili wachezaji wa uhakika, lengo ni kuwa na kikosi cha ushindani msimu ujao.


Stand ilipanda msimu uliopita na imeweza kumaliza katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 31 na kujihakikishia kushiriki ligi hiyo msimu ujao.

Mkurugenzi wa ufundi wa kikosi hicho, Muhibu Kanu, amesema kuwa msimu ujao lengo lao kubwa ni kufanya vema tofauti na walivyomaliza msimu huu, ndiyo maana wametenga kiasi kikubwa cha fedha ili kukisuka kikosi chao.
“Tumemaliza nafasi ya kumi kutokana na ugeni wa ligi lakini msimu ujao tunajipanga kufanya vizuri kwa kufanya usajili ambao utaifanya timu yetu kuwa na ushindani mkubwa kwa kutenga kiasi cha shilingi milioni 350.


“Lengo ni kupambana kufanya vizuri kama unavyofahamu timu zimeongezeka, hivyo tunahitaji kuwa makini hasa upande wa usajili. Tayari tumeanza mazungumzo na baadhi ya wachezaji wetu na hata wale ambao tulikuwa nao 
tunazungumza kuhakikisha tunaboresha mikataba na kuweza kuwaongezea,” alisema Kanu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic