May 4, 2015

TELELA
Unajua sababu ya Yanga kucheza soka la kuvutia licha ya kufungwa bao 1-0 na Etoile du Sahel? Ni kiungo Salum Telela kwani ndiye aliyewavuruga katikati.


Katika mchezo wa kwanza wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, Telela hakucheza kwani alikuwa majeruhi wa kifundo cha mguu lakini juzi Jumamosi alicheza na kuisumbua Etoile du Sahel.


Kwa mujibu wa Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm, Telela ndiye aliyechangia kwa kiasi kikubwa kuivurugia mambo mengi safu ya kiungo ya wapinzani wao.

“Ujue ndiyo kwanza anatokea katika majeraha, tuliwashtukiza kwa kumtumia kwani walikuwa hawamjui kabisa, hivyo hawakuwa na mpango wowote dhidi yake.

“Uliona jinsi tulivyowazidi katika kumiliki mpira kwenye kiungo na hata kasi yetu ilikuwa nzuri,” alisema Pluijm.

Kiungo wa Etoile du Sahel, Franc Kom alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 42 baada ya kumchezea rafu Simon Msuva na kuzidi kuidhoofisha safu yao ya kiungo.


Bao pekee la Etoile du Sahel lilifungwa dakika ya 25 na Ammar Jemal kwa kichwa akimalizia krosi safi ya Kom. Yanga inarejea jijini Dar es Salaam leo mchana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic