May 13, 2015

Washindi wa  simu za kisasa za Lumia Microsoft  kutoka nchi za Kenya, Uganda na Tanzania watakula ‘bata’ ya kutosha katika jiji la Cape Town nchini  Afrika Kusini kwa siku tatu.

Mshindi kutoka Tanzania, Richard Edward Mtango, Isaac Kinyera wa Uganda na Philip Mwaura kutoka Kenya watajumuika pamoja katika mji huo maarufu kama “Mother City”.

Yote hayo yalikuwa ni kupitia ile kampeni ya Make it Happen na zawadi zimekuwa zikitolewa kwa washindi mbalimbali.
Lengo ni kuwaonyesha watu mbalimbali ubora wa simu hizo za kisasa zaidi ambazo zinamuwezesha kupata kila anachotaka.

Programu kadhaa katika simu hizo zinaweza kuwasaidia wanamichezo kupata kila wanachohitaji na kwa ulahisi zaidi kutokana na ubora wa simu hizo.






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic