June 15, 2015


Uongozi wa timu ya African Sports ya Tanga, iliyopanda kucheza Ligi Kuu Bara msimu huu, umetamka wazi kuwa, upo kwenye mipango ya kutuma maombi kwa Klabu ya Yanga ili kupata ridhaa ya kumnasa beki wa timu hiyo, Edward Charles.


African Sports wamefikia hatua hiyo baada ya beki huyo kutokuwa na nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha Yanga kinachonolewa na Mdachi, Hans van Der Pluijm.

Meneja wa African Sports, Ahmed Bozinia, amesema wameona beki huyo ana uwezo mzuri na anaweza kuwa nguzo muhimu katika kukiimarisha kikosi chao kwenye mikiki ya Ligi Kuu Bara, hivyo wameamua kufikia uamuzi wa kufuata njia sahihi ili kumnasa.

“Mipango yetu inaendelea vizuri na sasa tunafanya utaratibu wa kutuma maombi kwa wenzetu wa Yanga ili watuachie Edward Charles, iwe kwa mkopo au kwa kumsajili moja kwa moja ili aitumikie timu yetu msimu ujao.

“Tumeona Yanga hawamtumii, lakini kwa uwezo alionao na umri wake, anaonekana kabisa kwetu atakuwa msaada kwa sababu atapata nafasi ya kucheza mara kwa mara. Kama tutamalizana vizuri na Yanga, basi atakuwa mchezaji wetu msimu ujao,” alisema Bozinia kwa msisitizo.


Charles alitua Yanga kwa mbwembwe msimu uliopita akitokea Ruvu Shooting, lakini amekuwa hapati nafasi ya kucheza mara kwa mara kikosini hapo kutokana na upinzani kutoka kwa mkongwe, Oscar Joshua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic