June 15, 2015


Kikosi cha Mwadui FC ya Shinyanga, imeeleza kuwa haihitaji kumuongeza mkataba mwingine mchezaji wa timu hiyo, Uhuru Selemani kutokana na kutoridhishwa na kiwango chake.


Uhuru, aliyewahi kuichezea Simba, amemaliza mkataba wake na Mwadui FC ambayo aliisaidia kuitoa Ligi Daraja la Kwanza msimu uliopita na sasa inatarajiwa kucheza ligi kuu.

Hadi sasa Mwadui imeshasajili wachezaji kadhaa ambao wataitumikia timu hiyo msimu ujao akiwemo Nizar Khalfan, Jabir Aziz, Shabani Kado, David Luhende, Paul Nonga, Rashid Mandawa pamoja na wachezaji wengi ambao tayari wameshapewa mikataba mipya.

Mwenyekiti wa Mwadui FC, Omary Khatibu, alisema idadi hiyo ya wachezaji waliowasajili ndiyo inayokamilisha usajili wa timu hiyo na kudai kuwa Uhuru hayupo katika mipango ya kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ kutokana na nafasi yake kujaa.

“Kwa sasa tayari tumejitosheleza, kwani mipango yetu ni kuhakikisha tunasajili wachezaji wasiozidi 25 ili kuimarisha kikosi.

“Uhuru hakuwa katika mipango ya kocha, kwani yeye ndiye aliyependekeza kuachana naye. Kwa kifupi, kwa sasa hayupo katika mipango ya timu,” alisema Khatibu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic