June 12, 2015

PAZI WAKATI SIMBA...
Uongozi wa Mwadui FC umefanikiwa kunasa saini ya aliyewahi kuwa kiungo wa Simba, Zahoro Pazi ambaye ndiye aliyefunga usajili wa timu hiyo huku ukimuajiri Habibu Kondo kuwa kocha msaidizi wa kikosi hicho akishirikiana na Kocha Mkuu, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.


Zahoro aliondoka Simba baada ya msimu wa 2013/14 akaelekea FC Lupopo ya DR Congo ambayo hata hivyo hakuichezea kutokana na kukosa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC), ikamlazimu arudi Bongo, akatua Polisi Moro ambayo hakuichezea kutokana na kukuta dirisha la usajili limefungwa. Baada ya kushindwa kucheza msimu wote uliopita, sasa ametua Mwadui FC.

Hadi sasa, kikosi hicho kimefanikiwa kusajili nyota wapatao kumi kutoka klabu tofauti huku kikiwaongezea mikataba wachezaji 13 walioipandisha timu.

Katibu wa Mwadui FC, Ramadhan Kilao amesema kwa sasa baada ya kumsajili kiungo huyo, hawataongeza mchezaji mwingine.

Alisema tayari nyota wao wapo kambini kwa ajili ya kuanza mazoezi huku akiahidi watasumbua sana msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.


“Leo tumefanikiwa kumalizana na kiungo Zahoro Pazzi ambaye amesaini mkataba wa mwaka mmoja, pamoja na Kocha Habibu Kondo aliyechukua nafasi ya Amri Said,” alisema Kilao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic