June 14, 2015



Mbio za Bagamoyo Historical Marathon zilizofanyika jana Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani zilitiafora kufuatia mchuano mkali ulioshirikisha taasisi na raia wa mataifa mbalimbali.

Katika michuano hiyo Klabu ya Mfuko wa Afya ya Jamii (NHIF) ambao huundwa na wafanyakazi wa mfuko huo kuwagalagaza wengine na wengi kuwemo kwenye kumi bora katika mbio za kilometa 5,10, na 21.

Wengine waliofanya vizuri kwenye mbio hizo ni raia wa kigeni kutoka barani Ulaya, Asia, Amerika na kwingineko.


Katika mbio hizo mshindi wa kwanza alikuwa Gabriel Gerald akifuatiwa na Panuel Mkungwa ambapo mshindi wa tatu alikuwa Dikson Marwa.

Washiriki wa mbio hizo walinufaika na kupimwa bure afya zao na madaktari kutoka NHIF nakupatiwa majibu yao hapohapo na kupatiwa ushauri wa kuboresha afya zao.  



Akifunga mashindano hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dk. Shukuru Kawambwa aliwapongeza washiriki wote kwani wameboresha afya zao na kuutangaza Utalii wa mji huo wa kale (Bagamoyo) jambo ambalo lilikuwa dhumuni la mbio hizo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic