June 14, 2015


Na Fahad Ally, Mwanza
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema anashangazwa suala la kocha mpya wa Simba kuwa gumzo sana na kusisitiza, watu wavute subira.

Akizungumza na SALEHJEMBE jijini hapa, Hans Poppe amesema Simba iko katika hatua ya mwisho kumalizana na kocha huyo.

“Vuteni subira kidogo, mambo yanakwenda kwa mpangilio. Si lazima kuwe na haraka kiasi hicho, tutawataarifu bila ya shida,” alisema.

“Najua mna hamu ya kumjua lakini ni suala ambalo linahitaji umakini. Najua nilishawaeleza tokea mwanzo kwamba anatokea Uingereza,” alisema.

Tokea kuondoka kwa Goran Kopunovic kumekuwa hakuna uhakika Simba inamchukua nani huku suala hilo likiendelea kuwa siri kubwa.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic