KISIGA (KATIKATI) WAKATI AKIICHEZEA SIMBA. |
Kiungo mkongwe,
Shabani Kisiga amesaini mwaka mmoja kuichezea Ruvu Shooting inayoshiriki Ligi
Daraja la Kwanza.
Kisiga aliyewahi
kung’ara na Simba na Mtibwa Sugar, amesaini kujiunga na Ruvu Shooting leo.
Msemaji wa Shooting,
Masau Bwire amesema kwa sasa tayari Kisiga ni mchezaji wao.
“Tunaendelea
kujiimarisha, kweli Kisiga tumemsajili kwa mkataba wa mwaka mmoja,” alisema
Masau.
Kiungo huyo
aliondoka Simba baada ya kushindwa kuelewana na uongozi na ilielezwa chanzo
alikuwa yeye baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu mara kadhaa kwa memba wa
benchi la ufundi.
0 COMMENTS:
Post a Comment