June 17, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, ametamba kwamba kwa maandalizi anayoendelea nayo sasa, yainaipa Yanga nafasi ya kufanya vizuri katika michuano ya Kombe la Kagame, ikiwezekana hata kutwaa ubingwa.


Yanga ni moja ya timu zitakazoshiriki kwenye michuano hiyo inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Julai 11, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Pluijm amesema mara kadhaa amekuwa akiulizwa kuhusiana na maoni juu ya timu yake katika Kagame lakini sasa anaona bora awatoe hofu mashabiki wa timu hiyo kwamba yeye pamoja na kikosi chake hakuna michuano wanayoihofia na kwamba wanafanya kazi moja tu ya kupambana na kuchukua kombe.

Aidha, Pluijm aliongeza kuwa timu yoyote inayotambua kuwa ipo kwa ajili ya kushindana, haiwezi kuwa na hofu.

“Najua kuhusu hii michuano na ninafahamu kuwa wapenzi wa Yanga wanalihitaji hili kombe pia, lakini nikwambie tu kwamba hata sisi tunajipanga na maandalizi yetu ya sasa pia yanajumuisha hiyo michuano, kwa hiyo watu wasiwe na wasiwasi, tutakwenda kupambana kwa ajili ya kuchukua kombe na si kingine.

“Kwa timu yoyote inayohitaji mafanikio na kujua inahitaji nini lazima ijipange na kwenda kulitafuta hilo kombe kama ilivyo kwetu Yanga, tutapambana kwa kuwa shida yetu ni hilo kombe na si kingine,” alisema Pluijm aliyeiongoza Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara katika msimu uliomalizika hivi karibuni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic