June 17, 2015


Wakali wa Golden State Warriors, wamefuta ndoto za mchezaji nyota wa kikapu LeBron James kwa kubeba ubingwa wa NBA.


Warriors wameifunga Cleveland Cavaliers kwa pointi 105-97  katika mechi yake ya mwisho ya faiinali na kubeba ubingwa.

Wakati Warriors wakichukua ubingwa huo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 40, LeBron ameupoteza kwa mara ya nne akiingia fainali bila kuuchukua.


Ushindi wa Warriors unaifanya iibuke na ushindi wa 4-2 katika mechi sita za fainali uliozikutanisha timu hizo. Cleveland Cavaliers walitaka kushinda mchezo wa jana ili kufanya matokeo yawe 3-3 na klusababishwa kuongezwa kwa mchezo mwingine wa fainali, lakini ikashindikana.

Stephen Curry wa Warriors ndiye ameibuka na tuzo ya mchezaji bora wa NBA wa michezo yote ya fainali pamoja na Andre Iguodala.

Pamoja na kuukosa ubingwa huo, LeBron ameonyesha ni mmoja wa wachezaji bora kabisa wa mchezo huo baada ya kuitoa Cleveland Cavaliers ikionekana timu isiyo na makali hadi kucheza fainali. Katika mechi hiyo ya mwisho alifunga pointi 32.







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic