July 24, 2015


Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, ametamka wazi kuwa wachezaji wenzake wa kikosi hicho walikuwa wakigombania kupiga penalti katika mchezo wa Kombe la Kagame, juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar dhidi ya Telecom ya Djibouti.


Katika mchezo huo ambao Yanga ilishinda kwa mabao 3-0, wachezaji wawili wa timu hiyo Amissi Tambwe na Simon Msuva walikosa penalti katika dakika ya 39 na 44.

Cannavaro amesema yeye ndiye mpigaji mkuu wa penalti wa timu hiyo lakini baada ya kukosa katika mchezo dhidi ya Gor Mahia, ndipo aliamua kujiweka pembeni katika mechi ya Telecom kwa kuwa wawili hao walikuwa wakitaka kupiga.

“Nilipokosa katika mechi ya Gor Mahia, kocha akaamua kutupa mazoezi ya penalti kabla ya mchezo dhidi ya Telecom, kila aliyepiga alionekana kuwa vizuri lakini mwisho wa siku ni kama ulivyoona.

“Siwezi kuwalaumu kwa kuwa penalti huwa hazina ufundi, hata wachezaji maarufu duniani wanakosa,” alisema Cannavaro.

Upande wa Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Mkwasa alisema hajui kilichotokea mpaka wachezaji wake wakakosa penalti hizo licha ya kuwa walifanya vizuri katika mazoezi.


Akizungumzia hali hiyo, Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, alisema yeye mwenyewe hajui kwa nini walikosa wakati mazoezini walifanya vizuri zoezi hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic