July 17, 2015


Kiungo mshambuliaji anayefanya mazoezi na Azam FC, Ryan Burge, raia wa Uingereza, ataikosa michuano ya Kombe la Kagame ambayo inatarajiwa kuanza kesho Jumamosi kutokana na kanuni za michuano hiyo kumbana.


Burge ambaye alitua nchini hivi karibuni na kuanza mazoezi chini ya Kocha Stewart Hall ambaye ni Mwingereza mwenzake, atakosa michuano hiyo kwa kuwa hajasajiliwa na kanuni za michuano hiyo inayosimamiwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), zinasema kuwa wanaoruhusiwa kushiriki ni wale waliosajiliwa na klabu husika.

Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd Maganga, ameliambia gazeti hili kuwa, mchezaji huyo alikuwa kwenye mipango ya kocha wao lakini ndiyo hivyo atakosa michuano hiyo kwa kuwa hawana jinsi.

“Tutawakosa baadhi ya nyota wetu akiwemo Burge licha ya kuwa yupo katika mipango ya kocha, bado hajasaini mkataba,” alisema Maganga.

Aidha, Msemaji wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, naye alisisitiza juu ya kanuni hiyo kwa kusema: “Wachezaji ambao wapo kwenye majaribio ya timu shiriki hawataruhusiwa kucheza Kombe la Kagame. Wanaoruhusiwa ni wale wenye mikataba rasmi.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic