July 17, 2015

Simba ipo kambini Lushoto, Tanga kujiandaa na msimu wa 2015/2016, kuna mengi yanaendelea kambini huko lakini kuhusu Kocha wa Simba, Dylan Kerr ni habari nyingine, sikia hii mpya aliyoitoa.


Licha ya kuwa kocha huyo ni mgeni nchini Tanzania, lakini ameonyesha kuwa ni mwepesi wa kuijua mitaa pindi anapotembelea au kukaa hata kama ni kwa muda mfupi, hiyo ni baada ya kumzidi mwenyeji wake katika kuzijua njia za Tanga.

Kerr ambaye pia amekuwa mstari wa mbele kuwaongoza wenzake wanapokuwa matembezini kama vile ni mwenyeji wa Tanga, mapema wiki hii alimzidi ujanja msaidizi wake, Selemani Matola wakati walipokuwa wakibishana juu ya njia ya kupita.

Ilikuwa hivi, Kerr na Matola walitembelea Gereza la Lushoto, walipokuwa wakirejea kambini kwao umbali wa kama kilometa nne kutoka gereza lilipo, walianza kubishana walipofika katikati ya safari juu ya njia ipi wapite ili wafike kambini kwao.

Baada ya kuvutana kwa muda, wakaona isiwe tabu, wakaamua kuwauliza wenyeji wao juu ya njia sahihi ni ipi kuelekea kambini kwao, Kerr akaibuka mshindi kwa kuwa njia waliyoelekezwa ni ile ambayo yeye ndiye alikuwa akitaka wapite.


Matola akawa mpole na safari ikaendelea kama kawaida huku wazawa hao wakibaki na maswali mengi jinsi Mzungu huyo alivyoweza kukariri njia kwa muda mfupi huku wengine wakijiuliza: “Au ameshawahi kufika Tanga?”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic