July 17, 2015


Mabeki wa kati wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani, wamejikuta wakipewa majukumu mazito na benchi la ufundi la timu hiyo, kisa kikiwa ni habari za safu kali ya ushambuliaji ya Gor Mahia ya Kenya.


Timu hizo zinatarajiwa kukutana kesho katika mechi ya ufunguzi ya michuano ya Kombe la Kagame kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar ambapo kumekuwa na taarifa kuwa safu ya ushambuliaji ya Gor Mahia ipo vizuri.

Baada ya habari hizo, Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, raia wa Uholanzi, aliamua kufanya kazi nzito kwa mabeki wake hao ili wawe fiti licha ya kuwa alikuwa akitoa mbinu mbalimbali kwa wachezaji wake wote kuelelekea kwenye mtanange huo wa ufunguzi.

Imeeleza kuwa mbali na mbinu wanazopewa lakini wametakiwa kuwa makini muda wote na kutofanya utani hata kidogo kwa kuwa watu wanaokutana nao ni washindani wakali na wajanja katika ufungaji.

Mmoja wa wachezaji wa Yanga amesema amesema kuwa, baada ya Pluijm kupata taarifa hizo, ndipo akawa na zoezi hilo kali.

“Kutokana na taarifa hizo, kocha alifanya mazungumzo na sisi na kututaka tuwe makini zaidi na tucheze kwa ushirikiano mkubwa lakini pia akawataka mabeki wote wakiwemo Yondani na Cannavaro, kuhakikisha hawafanyi makosa ya kizembe,” alisema mchezaji huyo.

Mechi hiyo itakuwa ya kwanza kuzikutanisha timu hizo mbili baada ya miaka 16, mechi ya mwisho kuzikutanisha timu hizo, Yanga ililala kwa mabao  4-0 na ilikuwa ni ya kutafuta mshindi wa tatu wa michuano hiyo iliyofanyika nchini Kenya.

Akizungumzia mchezo huo wa ufunguzi, Pluijm alisema: “Tunatambua kuwa wana kikosi imara lakini sisi pia tupo imara na hatutaidharau hata kidogo mechi hiyo na ndiyo maana tumepanga kuanzisha kikosi imara ili tupate ushindi.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic