July 19, 2015


Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr amepata nafasi ya kuiona Yanga ikicheza kwa mara ya kwanza katika mashindano.


Kerr raia wa Uingereza alikuwa uwanjani wakati Yanga ikipambana na Gor Mahia ya Kenya na kupoteza kwa mabao 2-1.

Kerr amesema, Yanga ni timu nzuri lakini si tishio kama alivyokuwa akisikia.

“Ni timu nzuri na inaweza kutoa ushindani, lakini si kama vile nilivyoambiwa,” alisema.

“Kwa kuwa nimeiona, nitaendelea kuangalia zaidi wanavyocheza. Pia ningependa kuiona Azam FC katika mechi zake maana ndiyo wapinzani wenyewe,.”

Kerr ameishaanza kuinoa Simba na ilikuwa kambini wilayani Lushoto kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam.


Chini yake, Simba bado haijaanza kucheza mechi za kirafiki kujiweka vizuri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic