July 19, 2015

Wakati Chelsea ikiwa nchini Canada kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya, Kocha wake, Jose Mourinho, amesema wala haoni shida namna timu nyingine zinavyokimbizana kwenye usajili.


Mourinho amesema Chelsea haiwezi kufanya usajili kwa kuangalia nani amefanya kitu gani.
“Kweli wenzetu wanatumia fedha nyingi katika usajili, lakini hiyo ni mipango yao na yetu ndiyo hii tunayofanya.

“Tunajua tunafanya nini, tunajua tunataka nini hivyo hatuna sababu ya kufuata mkumbo,” alisema.

Chelsea ndiyo mabingwa watetezi wa England na msimu huu ni kati ya timu zilizosajili wachezaji wachache zaidi huku Mourinho akisisitiza kutaka kubaki na kikosi cha msimu uliopita kwa zaidi ya asilimia 90.





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic