July 16, 2015


Mshambuliaji wa Simba, Hamisi Kiiza ametamba kuwa kikosi anachokichezea kitafanya vema kuliko wengi wanavyofikiria.
Kiiza amesema Simba imekuwa ikifanya maandalizi mazuri wakiwa wamejichimbia Lushoto.

“Wanaweza kuona kama hatujiandai, lakini tunafanya kila linalowezekana kuwa fiti kwa kufuata maelekezo ya walimu.

“Baadaye tutakuwa vizuri tu, acha kwanza tumalizie maandalizi,” alisema Kiiza.

Kiiza amerejea nchini baada ya kuwa ameachwa na Yanga na kutimka nchini.

Lakini Simba imemnasa na kumsajili kwa miaka miwili huku Simba wakiwa wana imani kubwa kuwa atakuwa tishio katika umaliziaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic