Kocha wa
Simba, Muingereza, Dylan Kerr, ameonekana kuwa na uchu wa timu yake kufunga
mabao mengi msimu ujao baada ya kila siku kuwafundisha wachezaji wake jinsi ya
kutumia nafasi za kufunga kila wanapozipata.
Simba
ambayo imepiga kambi wilayani Lushoto jijini Tanga, imekuwa ikifanya mazoezi
kwenye Uwanja wa Chuo cha Sekomu, ambapo Kerr amekuwa akiwakazania zaidi
wachezaji wake kufunga mabao ya mbali ambayo ni nje ya 18.
Kwa muda mrefu
katika kikosi hicho, mabao ya aina hiyo yalikuwa yakifungwa na Mganda, Emmanuel
Okwi aliyetimkia Denmark, moja likiwa ni lile alilomtungua kipa wa Yanga, Ally
Mustapha ‘Barthez’, msimu uliopita.
Lakini
hivi karibuni kocha huyo ameonekana kuanza kuwajenga wachezaji wengine kwa
kufanya hivyo.
Katika mazoezi ya timu hiyo, Kerr alionekana kutofurahia sana mabao ambayo yalikuwa yanafungwa ndani ya eneo la 18, akisisitiza wachezaji kufunga nje ya eneo hilo.
Kerr
ameiambia SALEHJEMBE kuwa, mchezaji si lazima afunge bao akiwa karibu na
goli bali ni kokote pale endapo tu akipata nafasi.
“Nawaandaa
wachezaji wangu si kwa ajili ya kufunga tu bali hata kukaba ili kabla msimu
ujao haujaanza, kikosi chote kiwe tayari kwa kupambana na wala sitaki kuona
huku pazuri halafu kwingine pabovu.
“Pia kwa
upande wa kufunga kama ulivyoona kila mchezaji namjaribu kufanya hivyo nikiwa
na maana kwamba hakuna wa kumtegemea mmoja, lakini nataka wafunge mabao hayo
kwa umbali wa mita 18 kama akipata nafasi ya kufanya hivyo.
“Kusubiri mpaka
afike karibu na goli ndiyo afunge si sahihi kwani tunaweza kukutana na
wapinzani ambao wao wamekuja kwa ajili ya kulinda lango lao tu,” alisema Kerr.







0 COMMENTS:
Post a Comment