Na Saleh Ally
USIPOSOMA vizuri na kunielewa, utaona kama ni mtu mchokozi sana, huenda nataka kukupa maumivu kwa makusudi tu kwa kuwa unaipenda sana Simba.
USIPOSOMA vizuri na kunielewa, utaona kama ni mtu mchokozi sana, huenda nataka kukupa maumivu kwa makusudi tu kwa kuwa unaipenda sana Simba.
Ukitulia
na kusoma ukanielewa, utagundua mengi sana kuhusiana na mpira wa Tanzania
unavyokwenda lakini mfano mzuri nimeamua uwe Simba ambayo ndiyo timu ya
Tanzania iliyokuwa ikitoka nje kucheza michuano ya kimataifa, inajulikana kazi
yake.
Simba ndiyo timu iliyoonekana kuwa ukombozi wa Watanzania katika mechi za kimataifa. Unakumbuka hadi leo hakuna rekodi ya mapokezi kwa timu yoyote kama ilivyopokelewa Simba mwaka 2003 wakati ikitua nchini kutoka Misri baada ya kuitwanga Zamalek.
Simba
iliifunga Zamalek kwa mikwaju ya penalti na kuivua ubingwa wa Afrika. Wakati
inafanya hivyo nchini Misri, Zamalek walikuwa ndiyo timu bora ya Afrika.
Nakumbuka
wakati huo, kwa mara ya kwanza nilimuona Augustin Lyatonga Mrema kwenye Uwanja
wa Taifa (Sasa Uhuru) akiwa pale kuipokea Simba pia. Lakini bahati mbaya pia
watu kadhaa mashabiki wa Simba walifariki dunia katika harakati za mapokezi
hayo.
KERR AKIKIANDAA KIKOSI CHAKE... |
Kabla
ya hapo, Simba nusura iweke historia ya aina yake baada ya kufika fainali ya
Kombe la Caf mwaka 1993, lakini ikafungwa na Stella Abidjan. Bado inabaki kwua
timu ya Tanzania kuwa na rekodi ya juu kabisa ya kucheza fainali ya michuano ya
Afrika.
Simba
ya 1993, ilikuwa inanolewa na Mtanzania, Abdallah ‘King’ Kibadeni. Simba ya
mwaka 2003, ilikuwa inafundishwa na Mkenya, James Agrey Siang’a ambaye
aliunganisha nguvu na Talib Hilal wakati wa kati ya Simba nchini Oman.
Hoja
yangu hapo ni kutaka kukuonyesha kuwa Simba za miaka hiyo, zikifundishwa na
makocha wa nyumbani au nchi jirani ndizo zinabaki kuwa na historia ya juu
kabisa hadi leo.
Simba
inayoandaliwa na Kocha Mwingereza, Dylan Kerr inaonekana kama ndiyo timu mpya
inayoanza kutambaa kwa kuwa ndani ya miaka mitatu inaonekana haina lolote
kabisa.
Kerr
ambaye ni mgeni, kamwe huwezi kumlaumu. Hauwezi kusema ameshindwa kwa kuwa
hatujaiona kazi yake ingawa unaweza kuwa huru kuweka hofu yako, kwamba kama
Milovan Cirkovic, Patrick Liewig na Goran Kopunovic walishindwa, yeye atakuwa
na nini kipya?
Kwamba
ukombozi wa Simba, irejee tena na kuwa timu tishio Tanzania Bara na Afrika
umekwama wapi? Kwa viongozi ambao kubadilishana kwao kijiti kumefanya mambo
yawe yanayumba tu, au makocha nao ni wana tatizo?
Simba
imefanya vizuri miaka kumi na ushee iliyipita, lakini leo haiwezi tena, tena
haisikiki kabisa na jina lake limebaki kuwa kubwa bila ya uwezo. Je, viongozi
wanaridhika? Inawezekana hapana.
Maana
tumeona juhudi zao kuhusiana na kambi, wamefanya kila linalowezekana. Lakini
kweli kila mmoja wao ana moyo wa dhati kuonyesha kweli kinachofanyika ni kwa
ajili ya klabu?
Hapa
ninakumbusha kuaminiana, kupendana na kuwakubali wengine kwa maana ya kufanya
mazuri kwa ajili ya klabu na si kuifanya sifa ya mmojammoja.
Matatizo
yanayoikuta Simba, ndiyo matatizo yanayoikuta Yanga. Kwani ile iliyokuwa chini
ya Abbas Gulamani ilifika mbali. Hii ya miaka hii chini ya Yusuf Manji,
ikiingia kwenye michuano ya Caf, mapemaa, inarudi nyumbani!
Nani
anajiuliza au kutaka kujua tiofauti ya zamani na sasa. Au nani anapiga hesabu
kutaka kujua kama kweli timu zetu hizi kubwa zinapiga hatua au ndiyo zimefika
na sasa zinaporomoja kurejea nyuma?
Yanga
na Simba za miaka ya 1990, zilionekana bora zaidi kuliko za sasa? Kama hivyo ni
kweli sasa tunakwenda wapi au unabaki kuwa muonekano wa jezi mpya lakini
uchezaji au viwango ni bora ya zamani.
Iko haja ya kujipima na kila
tunalofanya, bado kuna nafasi ya kuangalia rekodi za nyuma kwani zinatuhukumu
kwamba sasa tuna uwezo wa kifedha na teknolojia imeimarika, lakini timu zetu
zinafanya vibaya, hazina uwezo kama wa timu za zamani. Viongozi wanahusika? Au
wachezaji ni tatizo? Tujipime!
0 COMMENTS:
Post a Comment