Kampuni kubwa ya matairi ya Lassa ya
Uturuki, imeingia mkataba wa matangazo na kiungo mpya wa Barcelona, Arda Turan.
Turan raia wa Uturuki na naodha wa
timu ya taifa, amejiunga na Barcelona akitokea Atletico Madrid.
Lassa imeingia mkataba wa miaka minne
na Turan, sawa na ilivyo kwa Barcelona ambayo pia imeingia mkataba wa muda huo
na kampuni hiyo ya kuuza na kutengeneza matairi.
Kwa hapa nyumbani tanzania, kampuni ya
maarufu ya matairi inayojihusisha na michezo zaidi ni ile ya Bin Slum ya jijini
Dar es Salaam.
Misimu mitatu iliyopita, kampuni hiyo
iliidhamini Coastal Union hadi iliporejea Ligi Kuu Bara.
Lakini msimu uliopita, ikaweka rekodi
nyingine ya kudhamini timu tatu changa ambazo ni Mbeya City, Ndanda FC pamoja
na Stand United.
0 COMMENTS:
Post a Comment