September 5, 2015

DULE (WA PILI KUSHOTO) AKIZUNGUMZA NA MWINYI KAZIMOTO. KULIA NI DYLAN KERR NA SELEMANI MATOLA.
Kocha wa viungo wa Simba, Mserbia Dusan Momcilovic ‘Dule’, amesema ameshamaliza kazi ya kuwafanya wachezaji wake wawe fiti kupambana dakika 90 uwanjani kilichobaki ni utekelezaji tu.

Dule aliyeletwa na uongozi wa timu hiyo kuhakikisha wachezaji wanakuwa fiti, amefanya kazi na timu hiyo kwa muda usiopungua miezi miwili hadi sasa na amesisitiza kuwa vijana wake wameiva.

Kazi ya kocha huyo ilianzia Lushoto mkoani Tanga ambako Simba iliweka kambi kwa wiki mbili, kisha wakaenda Zanzibar halafu wakarejea Dar es Salaam kabla ya kurudi Zanzibar kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Dule, alisema kuna mabadiliko makubwa kwa wachezaji wake tangu alipowasili nchini na sasa na wapo vizuri katika nguvu na pumzi.


“Sasa wachezaji wapo sawa kwa fiziki uwanjani, wakiwa mazoezini wanafanya vizuri bado vile vitu wanatakiwa kuvionyesha kwenye mechi, kazi kwao,” alisema Dule.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic