September 5, 2015


Ili mawazo yao yawe katika mchezo wa leo Jumamosi na kuweza kufanya vizuri dhidi ya Nigeria, wachezaji wa Taifa Stars tangu jana asubuhi walipigwa stop kutumia Mitandao ya Kijamii ya WhatsApp na Facebook.



Taifa Stars inacheza na Nigeria kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mchezo wa Kundi G kuwania kufuzu kushiriki wa Kombe la Afrika 2017 Gabon.

Imeelezwa kuwa, Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa, anataka wachezaji wake wote wawaze mchezo huo, vinginevyo wakitumia mitandao hiyo, hawatakuwa makini na wanaweza kufungwa.

Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Hemed Moroco, ndiye aliyetoa agizo hilo kwa wachezaji wake jana asubuhi katika mazoezi ya mwisho ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, akiwasisitiza huduma ya mtandao wa ‘internet’ (data) katika simu zao.

“Zimeni data, mnatakiwa mpate muda mwingi wa kupumzika huku akili zenu mkizielekeza katika mechi ya kesho (leo), hivyo hamtakiwi kutumia WhatsApp hata Facebook.”


Wakati huohuo, kocha mshauri wa Taifa Stars, Abdallah Kibadeni, amesema: “Watanzania wasiwe na wasiwasi kwa mchezo huu, vijana wetu wapo vizuri, waje tu kuwashangilia uwanjani.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic