October 19, 2015


Katika kuhakikisha timu yake inatumia vyema mipira ya adhabu ya penalti, kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’, ameomba kupiga penalti zote zitakazotokea ndani ya uwanja.

Kauli hiyo, aliitoa mara baada ya kiungo mkabaji wa timu hiyo, Mzimbabwe, Thabani Kamusoko kukosa penalti katika mechi dhidi ya Azam FC iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1 i kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, juzi Jumamosi.

Huyo siyo mchezaji wa kwanza kukosa penalti kwenye timu hiyo, timu hiyo kwenye michuano ya Kagame iliwahi kukosa penalti tatu kwenye mechi mbalimbali, pia ilitolewa kwenye hatua ya robo fainali ya michuano hiyo na Azam kwa njia ya penalti.

Barthez alisema kuwa anashindwa kuelewa tatizo walilonalo na kusababisha washindwe kutumia vyema nafasi za penalti katika kufunga mabao.

Barthez alisema, kocha wao katika mazoezi kila siku hutoa programu kwa wachezaji wote jinsi ya kupiga penalti, hivyo anashindwa kuelewa sababu ya kushindwa kupiga kwenye mechi.

Aliongeza kuwa, yupo tayari kupiga penalti zote zitakazotokea uwanjani kama kocha wake atamruhusu, anaamini ana uwezo mkubwa wa kupiga na kufunga.
“Kama kufundishwa tunafundishwa kila siku na kocha wetu na wachezaji wanapiga na kufunga.

“Sasa nashindwa kuelewa tunapopata penalti wachezaji wanakosa, mimi nafikiri wachezaji wanashindwa kujiamini, hasa pale mtu anapoambiwa aende akapige penalti.

“Mimi ninaomba nipige penalti zote tutakazozipata, ninaamini nina uwezo mkubwa wa kupiga penalti,” alisema Barthez.


Pluijm alipotakiwa kuzungumzia hilo, alisema: “Mchezaji yeyote anaruhusiwa kupiga penalti pale inapotokea, kikubwa anachotakiwa ni kujiamini kabla ya kwenda kupiga.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic