Kiungo mshambuliaji wa
Yanga, Simon Msuva, amesikitishwa na kitendo cha wachezaji wa Azam cha kumtolea
maneno machafu ya kumdhalilisha katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliozikutanisha
timu hizo mbili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, juzi Jumamosi.
Msuva alidai
kuwa, wachezaji wa Azam walimtolea maneno machafu katika mchezo huo, mara baada
ya kufanyiwa faulo na kipa wa timu hio, Aisha Manula na kusababisha penalti
iliyopigwa na kiungo wa Yanga, Thabani Kamusoko lakini kipa huyo akaipangua.
Kitendo hicho
kiliwaudhi wachezaji hao wa Azam na kuanza kumtolea maneno machafu wakimshutumu
kuwa alijiangusha bila kuchezewa faulo na kipa huyo.
Maneno hayo
ambayo Msuva hakuwa tayari kuyataja, alidai kuwa yamemsononesha.
“Ile ilikuwa penati ya wazi kabisa kwa sababu
Aishi alinifanyia faulo ya wazi ambayo kila mtu aliona, sasa nashangaa kwa nini
wanitolee maneno machafu.
“Hata hivyo, sina
cha kuwafanya ila wajiulize kama wangekuwa wao wangefanyaje,” alisema Msuva
ambaye katika mchezo huo, aliingia kuchukua nafasi ya Malimi Busungu aliyeumia
baada ya kufanyiwa faulo zaidi ya 10 na wachezaji wa Azam.
0 COMMENTS:
Post a Comment