October 19, 2015


Muda mfupi baada ya kuvaa jezi ya Mbeya City na kucheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu Bara msimu huu akiwa na kikosi cha Mbeya City, kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ amepewa majukumu mazito na kocha wake, Meja Mstaafu Abdul Mingange.


Boban ambaye alicheza katika mchezo dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Sokoine, alionekana kutokuwa kwenye ubora wake, hali ambayo ilielezwa na kocha wake kuwa bado hajawa fiti na kuahidi kuwa kama akizingatia mazoezi basi anaamini atakuwa msaada mkubwa kwa timu hiyo.

Mingange amesema Boban ni mchezaji mzuri lakini hakuridhishwa na kiwango chake, ambapo amemtaka kupambana kurejea katika ubora wake uliozoeleka.
MINGANGE
“Boban bado hajawa fiti kwa asilimia zote, hivyo leo (juzi) hajaniridhisha sana pamoja na kwamba amecheza kwa kujituma na kuwafanya wenzake pia kuwa na bidii, najua atakuja kufanya vizuri zaidi ya leo.

“Tumefungwa leo kutokana na kupoteza umakini kipindi cha kwanza ila natumaini michezo ijayo nitafanya kila namna ili nihakikishe tunapata ushindi.

“Kwenye soka siku zote huwezi kuwa unacheza kwa historia hata kama tumefungwa na Simba watu bado wanatakiwa kuwa na imani na Mbeya City, kwani timu yangu ina upungufu mwingi ambao tutaufanyia kazi haraka iwezekanavyo,” alisema Mingange.

Kabla ya kutua Mbeya City, Boban alikuwa Uarabuni kwa ajili ya kucheza soka la kulipwa lakini hakufanikiwa kufuzu, kwa kuwa alikuwa ameshasaini mkataba wa kuichezea Mbeya City kabla ya ligi kuanza, amerejea nchini na kujiunga na timu hiyo kuitumikia kama mkataba wake unavyomtaka.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic