ANGALAU HAWA WANAFUNZI WALIIIONA KAZI YAKE NA KUMFUATA KUMPONGEZA, WADAU WENGI WA SOKA, WAKO KIMYA WANASUBIRI AHABARIBU.... |
Na
Saleh Ally
SOKA
ni mchezo unaojumuisha watu wa aina nyingi sana, wako wenye mapenzi ya dhati na
wengine wasiojali wala kufikiria hata kidogo, nature au asili ya mchezo wa soka
ni nini.
Katika
mashabiki wa soka, mjumuisho wa watu ni mkubwa sana, wako waelewa, wako wasiolewa
na wengine wanajiehusha makusudi!
Mashabiki
wa soka hasa hapa nyumbani, wengi wanasubiri kupaza sauti zao wakati wa makosa.
Lakini mambo yanapokwenda vizuri, kila mmoja hukaa kimya.
Hauwezi
kusema watu hawapendi mazuri, huenda wanapenda zaidi kukosoa kwa kudhalilisha,
kuumiza au kuudhi. Ndiyo maana ikitokea mchezaji kakosea uwanjani, suala lake
lazima litahusishwa na rushwa au haipendi timu hiyo.
Inawezekana
mchezaji huyo atahusishwa na mapenzi na timu nyingine au hata kuzushiwa aliwahi
kuonekana akiwa na kiongozi wa timu Fulani, ndiyo maana amefungwa.
Ajabu,
ni hivi, kila yule mchezaji anapokuwa akifanya vizuri, hakuna lawama lakini
hakuna pongezi, ajabu kabisa.
Nimeamua
kumzungumzia Ally Mustapha, kipa wa Yanga ambaye anajulikana sana kama Barthez.
Hakika yuko katika kiwango cha juu kabisa kipindi hiki.
Barthez
ameweza kumuweka ‘mkeka’ kipa Aishi Manula wa Azam FC ambaye kwangu namuona
ndiye kipa bora kabisa kinda katika kipindi hiki.
Barthez
ameitumikia Yanga kwa kiwango cha juu zaidi, umewasikia hata wanamsifia. Lundo
la mashabiki na wanachama, wameweka akiba ya mashambulizi siku atakapokosea
waseme alitokea Simba. Msaada wake wa sasa unaonekana ni ilimradi tu.
Achana
na ishu ya klabu, twende kwenye timu ya taifa, Taifa Stars. Barthez ameendelea
kuwa katika kiwango kizuri na huko Manula analazimika kusubiri kwa kuwa kipa
huyo mkongwe kwake yuko sawa kweli.
Kwa
kipindi hiki, hata kama si peke yake, lakini Barthez yuko katika kiwango cha
juu sana na amefanya kazi kubwa kuisaidia Stars kuiondoa Malawi na sasa
itakutana na Algeria kuwania kucheza Kombe la Dunia.
Ukiangalia
mechi ya kwanza wakati Taifa Stars inacheza na Malawi jijini Dar es Salaam,
utaona namna alivyokuwa mwokozi. Stars ilishinda kwa mabao 2-0, lakini hali
haikuwa nzuri na safu ya ulinzi na kiungo cha ulinzi kiliruhusu kupenywa zaidi
ya mara nane.
Barthez
aliokoa michomo mitatu iliyokuwa imelenga lango ambayo usingetemea hata kidogo
kama kweli aliiona. Kweli ni jukumu lake lakini ilikuwa ni kazi bora kabisa ya
kujivunia na kumsifia.
Mechi
ya pili ambayo Taifa Stars ilipoteza mechi ikiwa ugenini Malawi kwa kufungwa
bao 1-0 lakini ikasonga, mambo bado yalikuwa magumu.
Barthez
aliokoa shuti lililopigwa na mshambuliaji wa Malawi, hatua tano tu kutoka
langoni. Kama Stars ingefungwa bao katika dakika ya kwanza, hakika dakika 89
zilizobaki ‘ingefia ‘ Malawi kwa kuwa wachezaji wangechanganyikiwa
mapema.
Umakini
wa Barthez hata kama ndiyo kazi yake, umechangia Stars kufikia hapa ilipo. Kama
angekuwa pale langoni ni ‘kapu’, watu wanatupia tu, basi Stars ingepotea na
isingefanikiwa kuitoa Malawi.
Ukimuangalia,
Barthez ambaye ni mtaratibu alikuwa anaonyesha yuko tayari ya mchezaji na
alikuwa amenuia kuisaidia Stars kufikia hapo ilipo sasa na zaidi.
Kwa
kila alichokifanya BArthez kwa kuwa ni kizuri, si lahisi kusikia akizungumziwa
au anasifiwa kwa ubora wa kazi yake.
Akiharibu
ndiyo itakuwa gumzo, akiharibu ndiyo atatajwa sana. Watu watafungua vinywa vya
na kuanza kusema kuhusiana naye kwa mabaya.
Leo
nimeona huu ni mfano sahihi wa kuwakumbusha kwamba inapotokea mtu amekosea, pia
ni vizuri kuangalia kabla ya kukosea alikuwa akifanya vipi kuhusiana na
kupatia.
Yeye
ni binadamu, lakini mchezo wa soka makosa ni lazima. Kama utakuwa na watu
wanacheza tu bila ya kukosea, hata katika soka ingecheza timu moja ambayo
ingeshambulia mfululizo kwa dakika zote 90. Hivyo lazima tujifunze na vizuri
pia kujifunza na kupata uelewa wa unachokishabikia kuliko kuwa bendera fuata
upepo.
0 COMMENTS:
Post a Comment