Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Mbeya City
inatarajiwa kuikaribisha Simba, kesho Jumamosi katika Ligi Kuu Bara lakini ujio
wa kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ umeongeza nguvu kwenye kikosi cha Mbeya City
ambapo amesema anaamini timu yake itaibuka na ushindi.
Akizungumza
mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu yake hiyo, jana kwenye Uwanja wa
Sokoine, Boban alisema kwa jinsi alivyowaona wenzake katika muda mfupi,
anaamini ushindi utapatikana.
“Hii
imekuwa siku nzuri kwangu, nimegundua timu yetu ina kikosi bora, vijana wana
vipaji na uwezo mkubwa wa kucheza soka, binafsi hili limenishangaza na kunipa
imani kuwa Simba hawana nafasi kwetu Jumamosi, tutawafunga,” alisema Boban.
Wakati
huohuo, mchezo huo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine,
umesababisha kuwe na gumzo kubwa mkoani hapa, ambapo umekuwa ukizungumzwa
katika vijiwe vingi vya soka.
Kutokana
na hali hiyo, ulinzi ulikuwa mkali katika mazoezi ya Mbeya City ambayo ipo
chini ya Kocha Meja Abdul Mingange.
0 COMMENTS:
Post a Comment