October 1, 2015


Na Saidi Msumi, aliyekuwepo Morogoro
Mzunguko wa tano wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2015/2016 uliendelea tena katikati ya kwa michezo mitatu ambapo katika Uwanja wa Taifa Simba waliwakaribisha Stand United ‘Chama la Wanna’. Azam walivaana na Coastal Union wakati kule mjini Morogoro kulikuwa na kivumbi kati ya wakata miwa wa Turiani, Mtibwa Sugar dhidi ya mabingwa watetezi Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri.


Makala yangu siku ya leo nitaangazia mchezo namba 35 Mtibwa Sugar dhidi ya Yanga, mwamuzi akiwa ni Erick Okoka kutoka Arusha.

Sitalenga masuala ya kiufundi sana, badala yake ninaangalia usalama wa wachezaji uwanjani pale.

Mara nyingi nimekuwa nikilalamikia usalama wa mashabiki na mali zao hasa katika uwanja mkuu wa taifa pale klabu Simba na Yanga zinapokutana. Kumekuwa na usalama mdogo wakati wa kutoka mara mchezo unapokwisha na kufanyika vitendo vya wizi na unyang’anyi kwa mashabiki lakini afadhali sasa kidogo ulinzi unaridhisha kidogo.

Tuanze kuutazama mchezo kati ya Mtibwa sugar na Yanga ambapo baada ya mwamuzi Erick Onoka kupuliza filimbi kuhitimisha mchezo huo asilimia kubwa ya mashabiki wakaanza kuingia uwanja kushangilia ama hakika ilikuwa tafrani sio kwa wachezaji wala kwa waandishi wa habari ambao walikuwa wanawataka kufanya mahojiano na wachezaji au makocha wa kila timu hali ilikuwa ngumu kwa kweli.

Hili suala la mashabiki wa soka kuingia uwanjani si suala la kwanza kutokea katika Uwanja wa Jamhuri na hata Uwanja wa CCM mkwakwani ambapo kumekuwa na kasumba hii ya mashabiki kuingia uwanjani hasa pale mchezo unapomalizika.

Kwa baadhi ya watu wanaweza wakakuambia ni furaha na mapenzi waliyonayo kwa  wachezaji wao lakini huwezi kujua dhamira ya kila mtu kama kweli ana mapenzi na hiyo timu labda anataka kumdhuru tutajuaje?

Au hajaridhishwa na maamuzi ya mwamuzi na anataka kwenda kumdhuru? Mie nadhani sasa suala hili si la kufumbiwa macho hata kidogo ipo siku tutakuja kushuhudia wachezaji wakiwa wamejeruhiwa kutokana na tabia hii ya kijinga ya kuingia uwanja lakini pia inakuwaje walinzi mnaruhusu watu wasiohusika kukaa ndani ya uwanja?

Inatupasa sasa kuacha kujuana na sheria kufuata mkondo wake mana hakuna mtu aliyejuu ya sheria huku chini wabaki wanahabari na walinzi kuliko kuwa na mkusanyiko mkubwa ambao baadae unaanza kuingia uwanjani bila ya sababu ya msingi.

Pia tabia hii pia ipo kwa baadhi ya watu hasa vijana wadogo katika uwanja mkuu wa taifa ambao utawakuta wamejazana sehemu ya kutokea wachezaji hasa wakiwaomba jezi au viatu?Huu nao ni usumbufu mwingine kwani huwezi kumtafuta sehemu nyingine ili umuombe hivyo vitu mie nadhani sasa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) pamoja na vyombo vyenye mamlaka ya ulinzi na usalama vianze kutolea macho masuala haya kwa ukaribu wake mapema ndio mana nakukumbusha Rais wa TFF, Jamal Malinzi tusije tukaunda tume ya bure  kabisa baadae huko kuchunguza endapo tatizo litatokea uwanjani. Nawasilisha kwa leo.

0564-234573

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic