October 4, 2015



Mshambuliaji wa Royal Eagles ya Afrika Kusini, Uhuru Selemani amesema Watanzania wana nafasi ya kufanya vizuri nje ya Tanzania.


Lakini akasisitiza wataweza kufanya hivyo kama watajituma na kujiamini.

“Ninaamini nyumbani tuna vipaji vingi sana na wengi wana uwezo. Ninaona huku ligi ilivyo, ninaamini wengi sana wanaweza kufanya vizuri.

“Kila mara nasisitiza, wajiamini na kujituma, basi watafanikiwa,” alisema Uhuru ambaye yuko Royal Eagles kwa mkopo akitokea Jomo Cosmos.


Tayari matajiri wa Afrika Kusini, Mamelod Sundown wameanza kutupa jicho lao kwa kiungo huyo wa pembeni wa zamani wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic