November 15, 2015


Na Saleh Ally
Hivi karibuni Rais wa Simba, Evans Aveva alikwenda kushitukiza katika mazoezi ya Simba baada ya kutokea bila ya taarifa.

Simba ilikuwa ianajifua katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Aveva aliibuka na kujificha akashuhudia mazoezi yote ya Simba hadi walipomaliza.

Baada ya hapo benchi zima la ufundi likiongozwa na Kerr lilimfuata na kuanza kuzungumza naye. Wengine walikuwa ni Kocha Msaidizi, Selemani Matola, Kocha wa Makipa, Iddi Salim na Menaja, Abbas ‘Gazza’.

Siku chache baadaye, Matola alitangaza kuachia ngazi akieleza sababu kadhaa kuhusiana na Kerr ambaye aliamini wasingeweza kufanya kazi pamoja.

Baadhi ya sababu hizo ni Kerr kuonekana kutotaka kusikiliza ushauri wowote kutoka kwa Matola, kupanga kikosi bila ya kumshirikisha na wakati mwingine alisema kumtafutia fitina na wachezaji.

Ukirudi katika picha ambayo benchi la ufundi lilimfuata Aveva na kuanza kuzungumza naye siku ile, utagundua jambo ambalo huenda hatukuliona.

Wakati Aveva akizungumza na mabosi hao wa benchi la ufundi la Simba. Kila mmoja alionekana kuchangamka na kuzungumza naye.

Matola pekee ndiye alionekana muda wote akiwa ameinama yuko busy na simu yake na uchangiaji wake pia ulikuwa mdogo sana.

Inaelezwa siku chache baadaye, Matola alipata shutuma kwamba alikuwa akipeleka maneno kwenye uongozi na uvamizi wa Aveva ulihusishwa naye.

Picha ile ingeweza kusema maneno mapema sana kama uongozi wa Simba ungefuatilia kwa karibu na huenda pia lingekuwa jambo zuri sana kuanza kuokoa hali iliyokuwepo.

Ninaamini Simba ingeweza kuwaweka pamoja Kerr na Matola na kuwaeleza hali halisi na Simba ilikuwa inataka nini badala ya wao kufikia katika hali hiyo.

Inawezekana kabisa Simba waliona ni sahihi kumuacha Matola aende. Lakini suala la kujaribu kulimaliza suala hilo lilikuwa ni jukumu lao.

Kuondoka kwa Matola, kwangu naona alichelewa na wala hakutakiwa kusubiri mgogoro ndiyo aondoke. Badala yake aliatakiwa kufanya hivyo kwa ajili ya maendeleo yake kama kocha mwenye kipaji na uwezo wa kufanya vizuri akiwa kocha mkuu kijana.


Lakini msisitizo, uongozi wa Simba unapaswa kuwa mwepesi wa kung’amua mambo na kuyasawazisha kabla hayajafikia kuwa tatizo kubwa na wengine kujiuzulu kama ilivyokuwa kwa Matola.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic