November 9, 2015

KERR AKIWA NA SALEH ALLY MARA BAADA YA KUWASILI KATIKA KAMBI YA STARS
Na Saleh Aly, Johannesburg
Kocha wa Simba, Dylan Kerr leo ametembelea kambi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars jijini hapa.

Stars imeweka kambi kujiandaa na mechi ya kuwania kucheza Kombe la Dunia dhidi ya Algeria ambayo itapigwa Novemba 14 jijiji Dar es Salaam.

Kerr ametua katika kambi ya Stars na kusema amekuja kuiunga mkono Stars pia kuwaona wachezaji wake.

“Najivunia wachezaji wangu walioitwa katika kikosi cha Taifa Stars. Lakini niko hapa kuiunga mkono Tanzania kwa ujumla na wachezaji wote kwa kuwa ikifanya vizuri ni sehemu ya mafanikio ya Simba,” alisema Kerr.

Kerr alionekana mchangamfu, alizungumza na wachezaji mbalimbali lakini akaIsisitizia SALEHJEMBE kwamba Tanzania ina nafasi ya kufanya vizuri na inachotakiwa ni kujiamini.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic